January 19, 2014





 Na Baraka Kizuguto, Antalya
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania timu ya Young Africans jana imetoka sare ya kutokufungana (0-0) dhidi ya timu ya KS Flamurtari inayoshiriki Ligi Kuu nchini Albania katika mchezo uliofanyika usiku wa leo katika viwanja vya Side Stars Complex Manavgat Antalya


Ukiwa ni mchezo wake tatu tangu iweke kambi nchini Uturuki, Young Africans mpaka sasa imeshashinda michezo miwili dhidi ya Ankara Sekerspor 3-0, Altay SK 2-0 kabla ya kutoka sare leo.

Kocha Mkuu wa Young Africans mholanzi Hans Van Der Plyum leo alikua akikikiongoza kikosi chake kwa mara ya pili baada ya kukiongoza katika mchezo wa awali dhidi ya Altay SK.

Akiongelea mchezo wa leo kocha Hans amesema vijana wake wamecheza vizuri, timu zote ziliweza kucheza kwa nafasi, lakini kwa umakini wa walinzi wa timu zote ndio maana milango ilikua migumu kufunguka.

KS Flamurtari ni timu nzuri, awali hawakutegemea kama watapata ushindani mkali kutoka kwetu, lakini kadri mchezo ulivyokua ukiendelea walishangaa kuona tuna kikosi safi kilichokamilika.

“Washambulaji wetu walipata  walipata nafasi kadhaa  lakini hawakuweza kuzitumia vizuri, hali kadhalika mlinda mlango wetu Dida aliweza kuokoa hatari nyingi kipindi cha pili kutoka kwa wapinzani wetu” alisema Hans.

Young Africans imebakisha siku tano kabla ya kuanza safari ya kurejea nchini Tanzania tayari kwa mikikimiki ya Ligi Kuu ya Vodacom na Mashindano ya kimataifa.

Young Africans:
1.Deogratias Munishi “Dida”, 2.Juma Abdul, 3.David Luhende, 4.Mbuyu Twite, 5. Kelvin Yondani, 6.Frank Domayo, 7.Mrisho Ngasa/Said Bahanuzi, 8.Haruna Niyonzima, 9.Didier Kavumbagu/Saimon Msuva, 10.Emmanuel Okwi, 11.Hamis Kiiza

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic