January 6, 2014

KIBADENI (WA KWANZA KUSHOTO) WAKATI AKIWA KAZINI SIMBA, WANAOMFUATIA NI JULIO, NICO NYAGAWA NA DAKTARI WA TIMU.

Kocha Mkuu wa Ashanti United, Abdallah Kibadeni, amewamwagia sifa viongozi wa timu hiyo kwa kusema kuwa wanafanya kazi kwa kuzingatia utaratibu na mipaka ya kiutendaji, tofauti na alivyokuwa Simba.


 Kibadeni alisema hivi sasa anafanya kazi yake kwa amani zaidi bila ya presha na amepewa mamlaka makubwa zaidi na viongozi wa klabu hiyo.

Alisema hali hiyo itamfanya atekeleze mikakati yake ya maendeleo aliyojiwekea kwa utulivu zaidi ili timu hiyo iweze kufanya vizuri katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara utakaoanza Januari 25.
“Sina wasiwasi kwani hivi sasa nimetulia na ninafanya kazi yangu kwa amani zaidi bila presha ukilinganisha na nilivyokuwa Simba.

“Viongozi wa Ashanti United kila mmoja anafanya kazi yake kwa kufuata utaratibu, jambo ambalo sikuwahi kuliona katika timu nyingine ya ligi kuu,” alisema Kibadeni ambaye kabla ya kuinoa Simba alikuwa kocha wa Kagera Sugar.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic