January 6, 2014



Hali si shwari kwa baadhi ya wachezaji wa Yanga baada ya juzi Jumamosi uongozi wa timu hiyo kuwapa barua za onyo kuhusu utovu wao wa nidhamu na mambo mengine klabuni hapo.


Imeelezwa kuwa, juzi kiungo wa timu hiyo, Athumani Idd ‘Chuji’, alipewa barua ya kusimamishwa klabuni hapo kwa siku zisizojulikana huku nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Haruna Niyonzima, raia wa Rwanda, Jerry Tegete na David Luhende wakipewa za onyo kali.

Hata hivyo, uongozi wa Yanga umekuwa na siri kubwa kueleza ni utovu gani wa nidhamu uliosababisha Chuji akasimamishwa na wengine kupewa onyo kali.

Chuji alikasirika baada ya kutolewa uwanjani mara baada ya kumalizika kipindi cha kwanza cha mchezo wa Nani Mtani Jembe na kuondoka moja kwa moja kwenda nyumbani hali ambayo viongozi wameona ni dharau.

Chanzo makini kutoka ndani ya Yanga kimeliambia gazeti hili kuwa, viongozi wa ngazi za juu Yanga walikutana Ijumaa iliyopita, kujadili masuala mbalimbali ya klabu lakini kubwa lilikuwa juu ya wachezaji hao.

Kilisema kuwa kila mchezaji alijadiliwa kulingana na maisha anayoishi klabuni hapo pamoja na nidhamu yake kiujumla ambapo walikubaliana kumsimamisha Chuji, kisha wengine kupewa onyo kwanza kabla ya kuchukua hatua nyingine kubwa zaidi.

“Mipango ilikuwa ni kuangalia tatizo liko wapi Yanga, mara baada ya benchi la ufundi kusafishwa, lengo likawa kurudi kwa wachezaji ambapo tayari Chuji ameshasimamishwa na wengine wamepewa barua za onyo kali.

“Tegete, Niyonzima, Cannavaro na Luhende ndiyo wamepewa hizo barua, wameambiwa wajirekebishe mienendo yao wakiwa Yanga,” kilisema chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa jina gazetini.

Lakini wachezaji wote walikana kuhusiana na suala hilo na kwamba hawajapokea barua yoyote.

“Mi sijapokea barua ya onyo lolote, huo ni uongo, kama ningepewa ningekwambia.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic