January 29, 2014


Vita ya kuwania ufungaji bora wa Ligi Kuu Bara imenoga, Kipre Tchetche raia wa Ivory Coast amefikisha mabao 10 sawa na mshambuliaji wa Simba, Amissi Tambwe.


Tambwe raia wa Burundi alianza na kasi kubwa katika mzunguko wa kwanza, lakini hadi mzunguko wa kwanza unamalizika alikuwa na mabao hayo kumi.
Katika mechi ya kwanza ya Simba ya mzunguko wa pili wa ligi hiyo dhidi ya Rhino, Tambwe alitikisa nyavu mara mbili, lakini mara moja akawa ameotea na mara ya pili akamsukuma beki wa Rhino , hivyo kubaki na mabao yake 10.

Leo, Tchetche amefunga bao pekee la Azam FC katika mechi dhidi ya Rhino na kufikisha mabao hayo 10 za Mrundi huyo, hali inayoonyesha vita ya ufungaji mabao ndiyo kwanza kumekucha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic