January 29, 2014


Azam FC imeonyesha kama wakizubaa, basi inabeba ubingwa baada ya kuichapa Rhino ya Tabora kwa bao 1-0 na kupaa kileleni mwa ligi.


Kwa ushindi huo, Azam FC imesikisha pointi 33 na kuiteremsha Yanga yenye pointi 32 ambayo ilikuwa inaongoza hadi mwishoni mwa mzunguko wa kwanza.

Kabla ya kushuka uwanjani leo mjini Tanga, Yanga ilikuwa na pointi 31, pointi moja zaidi ya Azam FC, lakini sare dhidi ya Coastal imeifanya ishike nafasi ya pili.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Mbagala jijini Dar, bao pekee la mchezo huo lilifungwa na Kipre Herman Tchetche raia wa Ivory Coast.

Azam inayofundishwa na Kocha Omog raia wa Cameroon ilionyesha soka la taratibu lakini pasi za taratibu na uhakika na mwisho ikafanikiwa kushinda.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic