January 4, 2014



Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic amefunga safari kwenda kuiona Azam FC leo ikivaana na Spices katika mechi ya Kombe la Mapinduzi.


Logarusic ameiambia SALEHJEMBE kwamba amefanya hivyo kwa kuwa hajapata nafasi ya kuiona Azam FC ikicheza.

“Niliiona Yanga halafu nikaiona kwa mara ya pili wakati tukicheza nayo. Lakini sijawahi kuiona Azam FC,” alisema.
“Kwa kuwa ni wapinzani wetu kwenye ligi, ni lazima kuona wakicheza na kujifunza mambo kadhaa,” alisema.

Simba na Azam FC, kila moja imeanza mechi yake ya kwanza kwa kushinda.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic