January 4, 2014

MKWASA KAZINI SIKU YA KWANZA

Kocha Msaidizi wa Yanga, Boniface Mkwasa, amewataka wachezaji wake kuamini kazi imeanza.


Mkwasa ametaka kila mchezaji wa Yanga kujituma na kuamini wamerudi kazini.

“Baada ya mabadiliko, makocha kuondolewa utaona mambo yaliyumba. Lakini sasa tumeanza kazi na kila mmoja arudishe akili yake.

“Suala la tutaweka kambi wapi tunaliachia kwa uongozi lakini sisi ni kuongeza juhudi na umakini katika mazoezi,” alisema.
Mkwasa alianza kazi Yanga rasmi jana kwenye Uwanja wa Bora Kijitonyama jijini Dar.

Kabla ya kutua Yanga, Mkwasa ambaye si mara ya kwanza kuifundisha timu hiyo alikuwa akiinoa Ruvu Shooting.

1 COMMENTS:

  1. wafanye juhudi mana ndo wawakilishi wetu kwa mashindano ya mabingwa wa africa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic