January 8, 2014





Kocha Msaidizi wa Mbeya City, Maka Mwalwisye, ametaja kilichoiua timu hiyo katika michuano ya Kombe la Mapinduzi kuwa ni waamuzi.


Kocha huyo amesema uamuzi kwenye michuano hiyo ulikuwa mbovu na wengi wao walikuwa hawafuati sheria 17 za soka.
Mbeya City juzi ilishindwa kutamba mbele ya timu ya URA ya nchini Uganda baada ya kuchapwa bao 1-0 na kushindwa kuingia katika robo fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi.

Akizungumza na Championi Jumatano, kocha huyo alisema katika michuano hiyo kwa jumla waamuzi hawakuwa makini katika kutoa maamuzi, tena kwa kushindwa kuzingatia sheria.

Maka alisema, hata hivyo, wachezaji wa timu yake wamejifunza mengi kutokana na michuano hiyo na imeweza kuwasaidia kujiimarisha zaidi kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

“Uamuzi ulikuwa mbovu kutokana na kutozingatia sheria  za mchezo, kitu  kilichochangia hata timu kushindwa kufanya vyema kutokana na refa kutokuwa makini katika kuangalia nini anafanya pale uwanjani.

“Lakini kwa upande mwingine tumejifunza mengi na tumegundua wapi tunahitaji kurekebisha kabla ya kuanza mzunguko wa pili wa ligi na tuseme tumeweza kupata hata mechi kubwa kama kucheza na URA ya Uganda ambacho ni kipimo tosha kwetu.

“Na kwa jumla mashindano haya yametupa mwanga katika kuelekea mzunguko wa pili, japo tulikuwa hatujajiandaa kwa muda mrefu kwa sababu wachezaji ndiyo kwanza walikuwa wakitoka katika mapumziko,” alisema Maka.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic