January 8, 2014




Mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Emmanuel Okwi, amesema kambi ya timu hiyo inayotarajiwa kupigwa nchini Uturuki, itakibadilisha kwa kiasi kikubwa kikosi hicho na kukifanya kitetee ubingwa wake msimu huu.

Yanga ambayo ni bingwa mtetezi, inaongoza ligi ikiwa na pointi 28 na inatarajiwa kwenda Uturuki kesho Alhamisi kuweka kambi ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara.

Akizungumza na Championi Jumatano, Okwi aliyejiunga na Yanga akitokea Sports Club Villa ya Uganda, alisema mpaka sasa wachezaji hawazajazoeana, hivyo anaamini wakiwa huko mwalimu atatengeneza kombinesheni nzuri itakayoleta matunda katika timu hiyo.
Alisema anaomba sapoti kwa mashabiki ili waweze kufanikisha lengo lao la kutwaa ubingwa kwa mara ya pili mfululizo kwa kuwa hilo linawezekana iwapo tu watakuwa kitu kimoja.

 “Nafurahia sana kwa kuwa kambi inakuja wakati muafaka, itatusaidia kuimarisha kikosi chetu kwani kama unavyojua wachezaji wengine bado wapya, hivyo wanahitaji utulivu kujuana na kutengeneza kombinesheni nzuri.

“Ukweli naamini kuwa sapoti ya mashabiki wa Yanga inaweza kutufanya tukawa mabingwa msimu huu, hili ndiyo jambo zuri kwetu,” alisema Okwi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic