January 16, 2014


Simba imeendelea na mazoezi leo kwenye Viwanja vya Kawe jijini Dar.
Chini ya Kocha wake, Dravko Logarusic, Simba imefanya mazoezi lakini zaidi ilikuwa ni kutumia mipira.


Kocha huyo kutoka Croatia naye aliweza kuonyesha ujuzi wake na kufanya mashabiki wamshangilie.
Logarusic aliuchukua mpira na kupiga danadana huku akionyesha ujuzi hali iliyowavutia mashabiki wengi.


Simba imerejea jijini Dar es Salaam ikitokea Zanzibar ambako ilishiriki michuano ya Mapinduzi na kufikia hatua ya fainali na kupoteza mchezo kwa bao 1-0 dhidi ya KCC ya Uganda.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic