January 10, 2014



Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga, wametua salama nchini Uturuki na watafikia katika hoteli ya kifahari ya Sueno Hotels Beach katika Mji wa Antalya.



Safari hii Yanga wameonyesha jeuri ya fedha zaidi kwa kuwa watafikia katika hoteli hiyo ya kifahari yenye uwezo wa kuchukua zaidi ya watu 1000 kwa wakati mmoja.

Hoteli hiyo ya kifahari inamiliki viwanja vinne vya soka, vikiwemo vikubwa viwili. Lakini pia kuna viwanja vya tenisi na michezo mingine kama ya kuteleza kwenye maji.




Ufukwe wake una viti 1000 kwa ajili ya wateja wanaotaka kujipumzisha lakini kuna sehemu maalum kwa ajili ya kufanyia mazoezi.

Hoteli hiyo ya kifahari iko umbali wa kilomita tano kutoka maporomoko ya Manavgat ambayo hutembelewa na watalii wengi.

Umbali hadi kwenye Mji wa Antalya ni kilometa 70, kwenda Uwanja wa Ndege wa Antalya ni kilomita 60 lakini kuna sehemu mbalimbali za kitalii zilizo karibu yake kama Perge, Termessos na Aspendos.





0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic