January 29, 2014



Tiketi za elektronik zimeshindwa kufungua milango ya elektronik kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga na kuzua tafrani kubwa.


Kawaida mashabiki huzitumia tiketi hizo kufungua mlango, lakini walipojaribu leo ilishindikana na kusababisha zogo kwa waliokuwa wanataka kuingia uwanjani.

Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga umefurika mashabiki kibao waliojitokeza kushuhudia mechi inayoendelea kati ya wenyeji Coastal Union dhidi ya mabingwa Yanga.

Kutokana na hali hiyo ililazimu utaratibu wa kawaida uanze kutumika kwa mashabiki kuingia na tiketi kuchanwa kama kawaida, kitu ambacho hakikuwa kimepangwa.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic