January 29, 2014

JUMA NYOSSO AKIMDHIBITI SIMON MSUVA KWENYE UWANJA WA MKWAKWANI, LEO.

Na Mwandishi Wetu, Tanga
Sare ya bila mabao ndiyo majibu ya mchezo wa leo wa Ligi Kuu Bara kati ya wenyeji Coastal Union dhidi ya Yanga kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini hapa.

Coastal iliyoweka kambi nchini Oman kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara na Yanga ikaweka kambi nchini Uturuki, zimeshindwa kufungana huku kila upande ukishindwa kutimiza ulichoahidi.
Kila upande ulionyesha kupania mechi hiyo, lakini hakuna timu iliyopata bao ingawa kila upande ulipoteza nafasi za kufunga.
Kipindi cha pili, Yanga ilipoteza mwelekeo katika kiungo, Niyonzima na Domayo wakipoteana na kutoa nafasi kwa Haruna Moshi ‘Boban’ na Crispine Odulla kutamba na kusababisha hatari kadhaa.
Ngassa pia alipata nafasi ya kuifungia Yanga bao lakini akashindwa kuitumia nafasi hiyo na mwisho kukawa hakuna mshindi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic