January 10, 2014


MWENYEKITI WA SASA WA TASWA, JUMA PINTO


Na Walusanga Ndaki
UCHAGUZI mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (Taswa) unatarajiwa kufanyika Februari 16, mwaka huu jijini Dar es Salaam.


Taarifa iliyotumwa na katibu mkuu wa chama hicho imesema kuwa kikao cha viongozi wa Taswa kilichofanyika juzi  kimeamua kuwa mkutano huo ufanyike Februari 16.

Kikao hicho kilikubaliana kuwa uchaguzi ufanyike kwa katiba ya zamani kwani mchakato wa katiba mpya unaweza kuchukua muda mrefu, hivyo kusababisha viongozi waliopo madarakani kuendelea kukalia viti kinyume cha katiba, jambo ambalo si sahihi.

Kutokana na hali hiyo viongozi wapya watakaochaguliwa moja ya kazi zao kubwa itakuwa kuifanyia marekebisho makubwa katiba ya chama  hicho ili iende na wakati.
Pia kamati ya utendaji imeunda kamati ya uchaguzi na kumteua mwenyekiti wa zamani wa Taswa ambaye kwa sasa ni Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura, kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kusimamia Uchaguzi Mkuu wa TASWA, ambapo pia kutakuwa na wajumbe wengine wanne.

Wajumbe hao ni katibu mkuu wa zamani wa Taswa, Mwina Kaduguda, Peter Mwenda na wanahabari Isakwisa Mwaifuge na Mbonile Burton.

Fomu za kuwania uongozi zitaanza kutolewa Februari 10 hadi 14 mwaka huu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic