February 17, 2014


Kikosi cha Barcelona kimeshakwea pipa kwenda Mancheste, England kwa ajili ya mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya wenyeji wake Man City, kesho.


Picha iliyotupiwa kwenye mtandao wa Instagram na kiungo Cesc Fabregas imemuonyesha akiwa kwenye ndege.
Fabregas ameonekana akiwa na wachezaji wengine katika picha hiyo ambao ni
Alex Song, Carles Puyol na Gerard Pique wakionyesha kuwa tayari kwa ajili ya mechi hiyo ya ligi ya mabingwa hatua ya 16 bora.

Man City ndiyo tishio kwa upachikaji mabao kwa sasa, lakini Barcelona nayo inaonyesha kuanza kurejea kwa kuwa mechi yake ya mwisho iliitandika Rayo Vallecano mabao 6-0.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic