February 10, 2014


Bekiwa pembeni na nahodha wa Simba, Said Nassor ‘Chollo’, amemaliza dozi iliyomuweka nje ya uwanja kwa muda wa wiki tatu na sasa ameanza mazoezi mepesi.


Chollo alikumbwa na tatizo la nyonga alipokuwa mazoezini takriban wiki tatu na nusu zilizopita ambapo baada ya vipimo, alipumzishwa kwa wiki tatu kwa ajili ya matibabu.

Ofisa Habari wa Simba, Asha Muhaji, alisema wiki tatu za Chollo zimeisha jana na baada ya kurudi hospitali na kuangaliwa, ilibainika tatizo lake limekwisha, hivyo ameanza mazoezi mepesi.

Hata hivyo, Chollo atalazimika kwenda kwenye Hospitali ya Doctor’s Plaza kila baada ya siku mbili ili kuangalia maendeleo yake.

 “Zile wiki tatu za tiba na mapumziko za Chollo zimemalizika leo (jana), kwa hiyo amekwenda hospitali iliyomtibu mara ya kwanza ya Doctors Plaza na ameambiwa aanze mazoezi mepesi.

“Atalazimika kuangaliwa kila baada ya siku mbili, kama atakuwa amepona kabisa na kupewa ruhusa na daktari wa timu kuanza mazoezi, basi atajumuika na timu mapema iwezekanavyo kwa ajili ya maandalizi ya mechi zijazo za ligi,” alisema Muhaji.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic