February 4, 2014

CHANGA (WA TATU KUSHOTO MSITARI WA NYUMA) WAKATI AKIKIPIGA JKT RUVU

Bado tetesi zinaendelea kugubika kifo cha mshambuliaji nyota wa zamani wa Yanga, Omary Changa ambaye ameuwawa.


Mwili wa Changa uliokotwa hivi karibuni katika eneo la Jangwani jijini Dar es Salaam na haikujulikana nini kilitokea.
Lakini taarifa zinaeleza amenyongwa na nyingine zinaeleza amepata kipigo kutoka kwa watu wasiojulikana.
“Lakini tumeambiwa kuwa uchunguzi wa madaktari unaonyesha alishambuliwa ikiwa ni pamoja na kupigwa na kitu kizito usoni.
“Ila kila kitu kuhusiana na hilo tutapata leo na baada ya hapo tunaweza kufuatilia,” alisema ndugu yake wa karibu.

Changa aliwahi kucheza katika timu kadhaa zikiwemo JKT Ruvu, Moro United na Kagera Sugar na alikuwa kati ya mastraika noma.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic