February 4, 2014


Mshambuliaji Emmanuel Okwi amejiunga na kambi ya Yanga mjini Bagamoyo.
Okwi ambaye usajili wake umesimamishwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ameanza mazoezi na wenzake.


Akizungumza na SALEHJEMBE leo jioni, Okwi amesema ameanza mazoezi na wenzake baada ya kufanya pekee kwa zaidi ya wiki.
“Nilikuwa nikifanya mazoezi peke yangu, sasa nimeungana na wenzangu na tunafanya mazoezi pamoja,” alisema.

TFF imesimamisha usajili wake kwa madai kwamba kuna kesi tatu za msingi ambazo ni Simba kuishitaki Etoile du Sahel ikitaka kulipwa dola 300,000, Okwi kuishitaki timu hiyo na yenye pia imemshitaki Fifa.


Okwi alikuwa jukwaani akiishuhudia Yanga ikivunja mwisho wa msimu kwa kuifunga Mbeya City bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic