February 4, 2014


Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema kamwe hawawezi kuidharau Mtibwa Sugar.


Logarusic ambaye yuko mjin Morogoro tayari kwa mechi ya kesho ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar amesema watacheza kwa kujituma na kusahau ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Oljoro.

“Mechi iliyopita si yetu, tunaangalia mechi dhidi ya Mtibwa na hakuna atakayeidharau.
“Utakumbuka kabla ya kuanza mzunguko wa pili nilitangaza pointi zitakazokuwa ngumu sana, niliitaja Mtibwa Sugar.

“Ni moja ya timu imara na tunatarajia upinzani mkali sana,” alisema Logarusic.

Awali, Mtibwa Sugar ilicheza na Simba mechi ya kirafiki na timu hiyo chini ya Mzalendo, Mecky Maxime ikailaza Simba bao 1-0.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic