February 20, 2014


Kocha Msaidizi wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa yuko  uwanjani akiishuhudia Al Ahly ikipambana na CS Sfaxien ya Tunisia.

Mechi hiyo ya Kombe la Super Cup dhidi ya wababe hao wawili wa Afrika inapigwa muda huu kwenye Uwanja wa Jeshi jijini Cairo na mashabiki 20,000 wameruhusiwa kuingia.

Mkwasa amezungumza na SALEHJEMBE na kusema tayari ameanza kuishuhudia mechi hiyo.
“Niko uwanjani naishuhudia mechi, mambo mengine tutazungumza. Hapa bado haijaanza lakini baada ya muda mchache ujao timu zitaingia uwanjani,” alisema Mkwasa.

Yanga imemtuma Mkwasa kwenda kuisoma Al Ahly kama ambavyo timu hiyo ya Misri ilivyofanya kwa Yanga wakati ikicheza na Komorozine ya Comoro jijini Dar.
Yanga itaivaa Al Ahly katika mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika Machi Mosi jijini Dar na kurudiana jijini Cairo wiki moja baadaye.
Ndiyo maana uongozi wa Yanga ukaona ni jambo la muhimu kumpeleka Mkwasa na blog hii ilikuwa ya kwanza kueleza kuwa Yanga watatuma mtu Cairo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic