February 21, 2014


KWELI ushabiki wa soka ni hatari, mashabiki wa Simba na Yanga, juzi almanusura watwangane makonde katika mazoezi ya Yanga yaliofanyika kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers jijini Dar, kisa kikiwa ni ubishani juu ya usajili wa Emmanuel Okwi.


Katika mazoezi hayo, baadhi ya mashabiki walioonekana kuwa ni wa Simba waliovalia jezi nyekundu, walifika uwanjani hapo na kukuta mazoezi yakiendelea, ndipo wenzao wa Yanga wakaanzisha ubishi huo ambao ulizidi kukolea kadiri muda ulivyosonga.

Ubishi huo uliongezeka kiasi cha kufikia pande zote kuanza kutishiana, ambapo wa Yanga wengi walikuwa wakidai kuwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limefanya makosa kumzuia kucheza huku wenzao wa Simba wakidai kuwa Okwi hana uhalali wa kuichezea Yanga.


“Baba wa soka Fifa tayari ameshasema kuwa Okwi ni mchezaji halali wa Yanga halafu anatokea kidudu mtu eti anasema mpaka ajiridhishe,” alisikika shabiki mmoja wa Yanga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic