Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma
Mwambusi amesema wameweka mikakati ya kuhakikisha wanashinda mechi zote
zinazofuatia.
Mwambuzi amesema kikosi chake
kinachotaka ni ubingwa jambo ambalo linawezekana.
“Tofauti na watu wanavyofikiri, sisi
tunachotaka ni kutwaa ubingwa na si jambo jingine.
“Hivyo tunapambana na sasa tunataka
kushinda mechi zote zilizobaki, tunajua si kazi lahisi lakini tunapambana
vilivyo,” alisema.
Mbeya City iko katika nafasi ya tatu
katika msimamo wa Ligi Kuu Bara, Yanga ndiyo vinara wakifuatiwa na Azam FC.
0 COMMENTS:
Post a Comment