February 18, 2014


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ameondoka leo (Februari 17 mwaka huu) kwenye Cairo, Misri kujitambulisha kwa uongozi wa juu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).


Akiwa Cairo, Rais Malinzi ambaye alichaguliwa Oktoba 28 mwaka jana atakutana na Rais wa CAF, Issa Hayatou pamoja na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo Hicham El Amrani.


Akiwa mjini Cairo, Malinzi atapata nafasi ya kukutana na viongozi hao lakini pia kutembelea ofisi za makao makuu ya Caf. Pia atakutana na viongozi wa ngazi mbalimbali wa shirikisho hilo kubwa zaidi barani Afrika.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic