February 18, 2014


Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limewalalamikia wanafamilia watano wa mpira wa miguu kwa Kamati ya Maadili kuhusiana na udanganyifu katika mtihani wa utimamu wa miili ya waamuzi, lakini pia kuhusiana na suala la usajili wa mchezaji Emmanuel Okwi.


Riziki Majala na Army Sentimea ambao ni wakufunzi wa waamuzi, na Oden Mbaga na Samwel Mpenzu ambao ni waamuzi wanadaiwa kugushi nyaraka kuhalalisha mtihani huo kinyume cha taratibu.

Naye, Sabri Mtulla analalamikiwa ambaye ni mmoja wa maofisa wa shirikisho hilo, TFF inalala kwa madai ya kuidanganya Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji kuwa hakukuwa na pingamizi lolote juu ya usajili wa mchezaji Emmanuel Okwi huku akijua wazi kuwa jambo hilo si kweli.

Okwi alisajiliwa na Yanga akitokea SC Villa ya Uganda, wakati huo pia usajili wake ulikuwa bado una utata kuhusiana na suala la kesi yake na klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia iliyokuwa imemsajili kutokea Simba.

Baadaye TFF ilisimamisha usajili wake hadi na kutaka ufafanuzi wa uhalali wake kutokea kwa Shikirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).


Kwa mujibu wa kanuni, malalamiko hayo yamefikishwa kwenye Kamati ya Maadili ambayo itachunguza ili kujiridhisha kama yana msingi au la. Ikibaini kuna kesi ndipo walalamikiwa watafika mbele ya kamati hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic