Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) zimewaagiza wanachama wake, vyama
vya soka vya mikoa kuwapatia orodha ya klabu zote za mpira wa miguu
zilizosajiliwa katika mikoa yao.
Orodha hiyo inatakiwa kujumuisha
namba ya usajili wa klabu, viongozi waliopo madarakani kwa sasa pamoja na
mawasiliano yao (namba za simu na anuani za email) na eneo yalipo makao ya
klabu husika.
Kwa utaratibu huo, vyama vya mikoa
vitakusanya taarifa za klabu zinazocheza ligi ya mikoa, lakini wakati huo
vinatakiwa kuwasiliana na wanachama wake (vyama vya wilaya) kupata taarifa za
klabu zinazocheza ligi za wilaya na baadaye kuziwasilisha TFF.
Klabu ambazo taarifa zake zitakuwa
hazijawasilishwa TFF hadi Agosti mwaka huu hazitaruhusiwa kushiriki ligi ya
msimu wa 2014/2015 katika ngazi yoyote ile.
0 COMMENTS:
Post a Comment