Kwa mara nyingine bila ya kuwa na kipa mkongwe nchini, Juma Kaseja, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
(TFF) limetangaza kikosi cha wachezaji 22 kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya
kalenda ya FIFA dhidi ya Namibia (Brave Warriors) itakayochezwa Machi 5 mwaka
huu jijini Windhoek, Namibia.
Wachezaji walioitwa katika timu hiyo
ni makipa Deogratius Munishi (Yanga), Ivo Mapunda (Simba) na Mwadini Ally
(Azam). Mabeki wa pembeni ni Edward Charles (JKT Ruvu), Erasto Nyoni (Azam),
Hassan Mwasapili (Mbeya City) na Michael Aidan (Ruvu Shooting).
Mabeki wa kati ni Aggrey Morris
(Azam) na Kelvin Yondani (Yanga) wakati viungo ni Amri Kiemba (Simba), Athuman
Idd (Yanga), David Luhende (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Jonas Mkude (Simba)
na Mwinyi Kazimoto (Markhiya Sports Club, Qatar).
Washambuliaji ni Athanas Mdamu
(Alliance Mwanza), Haruna Chanongo (Simba), Khamis Mcha (Azam), Mbwana Samata (TP
Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Yanga), Ramadhan
Singano (Simba) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya
Congo- DRC).
Taifa Stars inayodhaminiwa na
Kilimanjaro Premium Lager itaingia kambini Machi 1 mwaka huu, kwenye hoteli ya
Accommondia inatarajiwa kuondoka Machi 3 mwaka huu kwenda Windhoek.
Wachezaji ambao timu zao zinacheza
mechi za mashindano ya kimataifa na ligi wikiendi hii wataripoti kambini mara
baada ya mechi zao kumalizika.
Shirikisho la Soka la Misri halikuwajumuisha wachezaji wa Al ahly kwenye timu ya Taifa kwa sababu wanakabiliwa na mechi za kimataifa. Misri watacheza na Bosnia tarehe 05 Machi 2014 jijini Vienna. Kwa nini TFF imewaita wachezaji wa Yanga?
ReplyDelete