February 11, 2014

Pamoja na kuwa na sifa ya kuwahi kuwapa wakati mgumu Al Ahly ya Misri, wakati huo akiinoa Berekum Chelsea ya Ghana, Kocha Mkuu wa Yanga, Mholanzi, Hans van Der Pluijm, amesema Waarabu hao si kazi ndogo.

Kocha huyo amesema kuwa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Komorozine, juzi, wachezaji wake walionyesha kizuri lakini wakivuka, kazi itakuwa ngumu zaidi.

Pluijm alisema wapinzani wao Al Ahly, watakaocheza baada ya kuvuka dhidi ya Komorozine ya Comoro ni wazuri na wazoefu.

“Tumefanya vizuri mechi ya kwanza tukiwa nyumbani, japo bado tunatakiwa kwenda Comoro na baada ya hapo tunakutana na Al Ahly ya Misri. Ile si timu ya kubeza kwani naifahamu vizuri kwa sababu awali niliwahi kukutana nayo.

“Kikosi chetu lazima tuendelee kujipanga kwa ajili ya mchezo huo kwa sababu lengo letu kubwa ni kuhakikisha timu yetu inafika mbali katika michuano hii.


“Nguvu zetu tunaelekeza kwenye mchezo uliopo mbele yetu. Lazima tuhakikishe tunajiandaa vyema,” alisisitiza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic