February 11, 2014


Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage na wachezaji wa Simba, jana walijifungia kwa takribani saa nne katika makao makuu ya klabu hiyo barabara ya Msimbazi jijini Dar es Salaam.


Rage aliitisha kikao hicho cha wachezaji pamoja na benchi la ufundi kutaka kujua kilichosababisha kuboronga mechi mbili mfululizo kwenye Ligi Kuu Bara.

Simba ilitoka sare na Mtibwa Sugar na baadaye kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Mgambo JKT, hali iliyosababisha Rage kutaka kuzungumza nao.

Mkutano huo ulianza ulianza  Saa 7:00 mchana na kumalizika  saa 10 na ushee jioni na Rage alizungumza mambo kadhaa, likiwemo suala la kutaka kujua kama wachezaji wana matatizo au kudai.

Pamoja na wachezaji, wengine waliohudhuria ni wajumbe wa kamati ya utendaji na SALEHJEMBE ilipata taarifa za uhakika kuhusiana na kila kilichokuwa kinaendelea.

 “Wachezaji walimtaka mwenyekiti kushughulikia madai yao wanayoidai klabu hiyo ikiwa ni pamoja na kuwalipa fedha zao za mshahara kwa wakati.
“Lakini pia waligusia suala zima la kufokewa na kocha Logarusic, Rage aliahidi kulishughulikia suala la mshahara, lakini kuhusiana na suala la kocha alionekana kutotaka kuliingilia sana kwa kuwa kocha pia lazima afanye kazi yake,” kilieleza chanzo.

“Lakini wachezaji pia walisisitiza kufungwa na sare dhidi ya Mtibwa ni sehemu ya hali ya kimchezo na kuahidi ataona katika mechi dhidi ya Mbeya City,” kilieleza zaidi chanzo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic