March 3, 2014


Na Saleh Ally
HII si mara ya kwanza kusikia mashabiki wa soka wamefanya vurugu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kusababisha uharibifu mkubwa kwenye vifaa vya uwanja huo.

Haraka labda nifanye hivi, napenda kuwakumbusha mashabiki na watu wengine kuwa Uwanja wa Taifa ndiyo bora na wa kisasa zaidi kuliko vingine vyote katika ukanda wa Afrika Mashariki. 

Nitakutakia nchi ili ukumbuke vizuri, Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, DR Congo, Ethiopia na Sudan.

Inawezekana kwa kuwa mimi na wewe ni Watanzania, basi tunakuwa wagumu kuamini kama kitu kikiwa Tanzania kinaweza kuwa bora kuliko vilivyo sehemu nyingine, lakini kwa uwanja tulio nao, hiyo ndiyo habari ninayokupa na kama ulikuwa unalijua hilo, si vibaya, nimekukumbusha.

Hao Al Ahly wanaotokea Misri, nchi liyoendelea sana kimatafa katika michezo, hawa uwanja wao pamoja na kwamba ni mkubwa sana, lakini si bora kama ulivyo huo wa Taifa ambao umefunikwa juu na ni wa kisasa kuliko wa kwao ambao umekuwa ukiongezewa viraka mara kadhaa.

Kuna viwanja katika nchi mbalimbali barani Ulaya, pamoja na kuwa maarufu havina ubora wa Uwanja wa Taifa, hakika Watanzania wana kila sababu ya kujivunia na kuulinda uwanja huo. Lakini ajabu kabisa, kumekuwa na makundi ya mashabiki wanaofanya juhudi za kuuharibu.
Takribani mechi nne, nimeshuhudia eti, mashabiki wenye hasira kali wameamua kung’oa viti na kuwarushia wengine. Kitu ambacho kama umetuliza akili zako, utaona kama ni ndoto au wanaofanya si watu wenye akili timamu badala yake ni wenye matatizo kisaikolojia.
Suala hili si sahihi, mtu ambaye hatakiwi kung’oa viti hivyo anapaswa kuonyesha upendo na uzalendo kwa mali za taifa lake, hadi asombe sifa nilizozitoa kuhusiana na uwanja huo, badala yake anapaswa kujitambua.
Uwanja huo ni mali ya Watanzania, mimi, wewe na yule na tunapaswa kujivunia, kuwa tuna kitu bora na tunapaswa kukitunza. Lakini ajabu kila zinapotokea tafrani uwanjani, mashabiki hung’oa viti na kuanza kurushia, vinahusika vipi.

Inakuwaje mtu mwenye hasira lazima ang’oe viti? Viti vinahusika nini kati ya shabiki wa Yanga na Simba au timu nyingine? Au ndiyo ule mtindo kwamba mtu anapokuwa katika kundi la watu anataka kuwaonyesha yeye ni hatari sana akikasirika na anaweza kung’oa viti.

Kama hali hiyo itaendelea mwisho wake nini au anayefanya vile anafaidika nini? Kwanini kama mashabiki wanazozana au kugombana, basi wasifanye hivyo bila ya kugusa viti? Wanajua wanaingiza hasara kiasi gani kila wanapofanya hivyo?

Mkatika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga dhidi ya mabingwa Al Ahly, mashabiki wa Yanga na Simba walipigana mara kadhaa. Kila hasira ziliyempanda alitumia viti vya uwanja huo kama silaha ya kupoteza hasira zake au kumuumiza mpinzani wake.
Wakati fulani nilimshuhudia shabiki mmoja wa Simba, akijaribu kumzuia shabiki mwenzake asirushe kiti alichokuwa nacho mkononi kwenda upande wa mashabiki wa Yanga kwa kuwa akifanya hivyo, wale wa Yanga nao wangejibu wakati yeye alikuwa na mtoto mdogo.

Hatari ya yule mtoto kuumizwa lakini ni dalili ya kusababisha dada na mama zetu wahofie kwenda uwanjani sababu ya wapuuzi wachache wanaoamini ni mashabiki wa kweli wa mpira, kumbe ni waharibifu na wahujumu uchumi wanaotaka kuturudisha nyuma. P
ia nilimuona shabiki wa Simba akiwa amelazimika kuangalia mpira huku akiwa amejifunika na kiti kichwani na kilichokuwa kimeng’olewa. Hofu yake ilikuwa ni hivi, wakati anaangalia mpira, kiti kinaweza kuvurumishwa kutoka upande wa Yanga na kikatua kichwani mwake.

Ushabiki wa kishamba, ushabiki wa kizamani, watu wa kizamani na wenye mawazo hasi yasiyokuwa na gia songa. Wanataka Tanzania ibaki ileile yenye viwanja ambavyo mashabiki wamekuwa wakikaa chini. Si vizuri, lakini wanaweza kujipima hivi; wale wanyama ambao unawawekea chakula kwenye sahani, wao wanatoa na kulia chini.

Watu wa usalama bado hawajawa wakali vya kutosha, kuna kila sababu ya kuongeza nguvu na kuwamaliza watu wa namna hiyo. Sheria ichukue mkondo wake, wanaonyesha akili zao zinashindwa kutambua kuwa matumizi ya viti ni yapi. Basi hakuna haja ya kuwafundisha na badala yake adhabu iwakute.

Washughulikie, ikiwezekana mmoja au watakaopatikana na hatia wafikishwe kizimbani kwa upuuzi wanaofanya ili iwe mfano. Mkiendelea kuwaachia, wataufanya uwanja huo uwe na gofu kwa kisingizio cha hasira. Kama kweli ni watu waliokasirika na wanashindwa kujitambua katika kipindi hicho, mbona hawatoi simu zao mifukoni wakawaponda mashabiki wanaowabugudhi. Watu hawa hawatufai kwenye jamii yetu.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic