March 2, 2014


Simba imeamka baada ya kuichapa Ruvu Shooting kwa mabao 3-2 katika mechi ya Ligi Kuu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.


Simba imekuwa ikisuasua, katika mchezo wa leo ilipata mabao yake mawili kupitia kwa Mrundi Amissi Tambwe.
Haruna Chanongo alifunga bao la tatu kwa Simba, lakini bado ilionekana safu yake ya ulinzi haikuwa makini sana.

Ruvu Shooting ambayo iliipa Simba presha kubwa ilifunga mabao yake mawili kupitia kwa Said Dilunga na Jerome Lambele na nusura wanajeshi hao wasawazishe.

Kwa ushindi huo Simba imefikisha pointi 35 lakini katika inaendelea kubaki katika nafasi ya nne, chini ya Azam FC, Yanga na Mbeya City.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic