April 9, 2014



Mambo bado ni magumu mkoani Shinyanga, uongozi wa timu ya soka ya Mwadui ya mkoani humo, umedai kuwa upo tayari kutumia mamilioni ya fedha mpaka makao makuu ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) ili kuhakikisha unapata haki yake ya kushiriki ligi kuu msimu ujao, kama Rais wa TFF, Jamal Malinzi alivyofanya wakati anataka uongozi huo.


TFF wameitangaza Stand kuwa ndiyo imepanda daraja baada ya kushinda rufaa yake na kupewa pointi tatu za mezani kutokana na madai ya Kanembwa kuchezesha wachezaji waliosajiliwa wakati wa dirisha dogo kwenye mechi yao ya mzunguko wa kwanza iliyorudiwa.

Hali hiyo imewaweka katika wakati mgumu viongozi wa Mwadui ambao walikuwa na matumaini makubwa ya kuiona timu yao hiyo ikishiriki michuano ya ligi kuu msimu ujao.

Kocha Mkuu wa Mwadui, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, alisema uongozi wa timu hiyo umejipanga kuhakikisha haki yao inapatikana kwa gharama yoyote ile.
Alisema wanatarajia kuwasilisha rufaa yao TFF, muda wowote kuanzia sasa ili kupinga uamuzi wa shirikisho hilo kuizawadia Stand United pointi tatu za mezani na kama litashindwa kuwapa haki yao, basi watatinga Fifa.
“Tunatarajia kupeleka TFF rufaa yetu muda wowote kuanzia sasa ili kudai haki yetu kwani hatupo tayari kuona inapotea hivihivi kwa sababu ya maslahi ya watu wachache.
“Tutafuata taratibu zote mpaka kuhakikisha inapatikana na ikiwezekana tutafika Fifa ili kuipata kama alivyofanya Malinzi alipokuwa akitaka kuingia TFF, uongozi wetu umesema kuwa upo tayari kwa jambo hilo na umejipanga kwa kila kitu ili kuhakikisha tunapata haki yetu hiyo,” alisema Julio.
Pointi moja tu ndiyo iliyoinyima Mwadui tiketi ya kushiriki ligi kuu msimu ujao ambapo kabla ya Stand United kupewa ponti tatu za mezani, Mwadui ilikuwa ikiongoza kundi lake kwa pointi 31 na Stand United ilikuwa ya pili (pointi 29).


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic