April 9, 2014


Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm, amesema mchezaji Emmanuel Okwi hayupo kambini na suala lake lipo juu ya uwezo wake na hawezi kumtumia kwenye mechi ya leo dhidi ya Kagera Sugar.


Pluijm amesema mbali na Okwi, kuna wachezaji wengine kadhaa hawapo, lakini yeye anaendelea kupambana na wale waliopo.

Baada ya mchezo wa Mgambo na Yanga jijini Tanga kuchezwa na timu hiyo kufungwa, baadhi ya wachezaji wa timu hiyo akiwemo Emmanuel Okwi, Kelvin Yondani, Athuman Idd ‘Chuji’ na Haruna Niyonzima hawajaonekana tena uwanjani kuitumikia timu hiyo na hata kwenye ushindi mnono wa mabao 5-1 dhidi ya JKT Ruvu hawakuwepo dimbani.

Kocha huyo alisema sababu za baadhi ya wachezaji wake kutokuwepo kama Okwi zipo juu ya uwezo wake, hivyo hawezi kuzungumza lolote kuhusiana na wachezaji hao lakini kwenye kikosi chake leo hawawezi kucheza.
Pluijm alisema kuwa ataendelea kuwatumia wachezaji wake haohao waliopo kambini na si vinginevyo kwa sababu hao ndiyo wanaofanya mazoezi na siyo ambao wapo nje ya kambi.
“Suala la mshambuliaji Emmanuel Okwi kutokuwepo kambini sijui ni kwa nini, sababu zipo juu ya uwezo wangu, siwezi nikasema vitu ambavyo sivifahamu.
“Lakini kikubwa ni kwamba mimi ninaangalia wachezaji waliopo hapa kambini, hata katika mchezo ujao nitawatumia hawa waliopo hapa na si nje ya hapa,” alisema Pluijm.
Wakati huohuo, daktari wa timu hiyo, Juma Sufiani, alisema kuwa, kwa sasa kikosi hicho kina wachezaji wagonjwa wawili ambao ni Haruna Niyonzima na David Luhende ambao walikuwa wanasumbulia na malaria lakini afya zao zimeanza kuimarika kwa kiasi kikubwa.
“Haruna Niyonzima na Luhende ndiyo wagonjwa lakini wanaendelea vizuri na wameanza mazoezi mepesi binafsi kisha wataungana na timu,” alisema Juma.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic