April 9, 2014

MAN CITY
Na Saleh Ally
MOJA ya hesabu nzuri wanazozitaka makocha wengi makini kwenye soka ni kuona timu zao zinaanza kufunga mabao katika mechi wanazocheza.


Kawaida, timu inapoanza kufunga inakuwa na nafasi nzuri ya kufanya vema katika mechi husika. Kupata bao, hesabu zinakuwa nzuri zaidi na kinachofanyika ni kulilinda na kuongeza bao jingine.

Iwapo timu itafanikiwa kufunga bao la kwanza, halafu ikaongeza, tayari inakuwa imejiweka katika nafasi nzuri ya kushinda mechi hiyo.

Lakini kila timu inapoongeza bao, lazima umakini kwenye ulinzi uongezeke kwa kuwa kama wataruhusu wapinzani kusawazisha, mara nyingi wanaosawazisha ndiyo wanaopata nguvu zaidi, hivyo kupoteza inakuwa rahisi kwa waliofunga bao la kusawazisha..
 
CHELSEA
Katika Ligi Kuu England, timu zinazoamini au kuitumia vizuri hesabu hiyo ya kuanza kufunga ndiyo zinazoonekana kufanya vizuri zaidi hata kwenye msimamo.

Hii inaonyesha kiasi gani unapoanza kufunga, inakuwa kweli ni nafasi nzuri ya kufanya vyema katika dakika 90 kwa kuwa kufunga ni sehemu ya kumchanganya mpinzani.

Liverpool ndiyo wanaonekana kuwa wajanja wa kuwahi kufunga katika mechi zao nyingi walizocheza wakifuatiwa na timu za Man City, Arsenal, Chelsea na Everton.

Liverpool:
Wakali hao kutoka Anfield ndiyo wanaonekana wanaiweza zaidi kazi hiyo kwa kuwa katika mechi 33 walizocheza za Premiership msimu huu, 25 walikuwa wa ndiyo wa kwanza kufunga.

Katika mechi hizo 25 walizoanza kufunga wanaonekana kuwa na wastani wa juu kwani hadi mwisho wa dakika 90 walifanikiwa kushinda mechi 21, mbili wakatoka sare na kupoteza mbili.

Iko hivi; yaani zile mbili walianza kufunga, wakapoteza baada ya wapinzani wao kusawazisha na zile mbili walianza kufunga, wapinzani wakasawazisha na kushinda.

Man City:
Katika mechi 31 za Premiership, Man City wameanza kufunga katika michezo 24 na walifanikiwa kushinda katika mechi 20, wakipoteza mbili na kutoka sare mbili.

Utaona wastani wa Liverpool na City hauna tofauti kubwa, pia ndiyo timu zinazopewa nafasi kubwa kutwaa ubingwa na hii inaonyesha mpango wa kuanza kufunga unasaidia sana.
Chelsea:
Vijana wa Jose Mourinho ni wabishi kweli, katika mechi zao 33 za ligi, 21 walianza kufunga na wakaweka rekodi nzuri ya kushinda 18 zote walizoanza kupata bao.

Hata hivyo, nao wakataleza, kuwa pamoja na kuanza kufunga, walishindwa kupambana na mwisho wakatoa sare mechi mbili na kupoteza moja tu ambayo ni rekodi nzuri na inaonyesha kuwa Chelsea wakianza kufunga ni nadra sana wapinzani kusawazisha na kupata sare au ushindi.

Arsenal:
Ingawa wamepewa jina kuwa ni wazee wa ‘rivasi’, lakini bado vijana wa Arsene Wenger wanajitutumua na kutoa ushindani mkubwa kwenye Ligi Kuu England maarufu kama Premiership.
Katika mechi 33 walizocheza, Arsenal walianza kufunga katika mechi 20 na wakaonyesha pia ni wazuri kama wakitangulia. Kwani wamepoteza moja tu na sare moja pia.

Hivyo Arsenal ni kati ya timu ambazo zikitangulia kufunga, ujue una kazi kubwa ya kugeuza mambo ili kupata sare au kuwafunga.

Everton:
Msimu huu wamezidi kuonyesha ni wazima kweli, katika mechi 32, wao wameanza kupata bao katika mechi 18 na kati ya hizo wameshinda 16, wakatoka sare moja halikadhalika kupoteza moja tu.

Man United:
Jamaa bado wanajikongoja kwenye Premiership na balaa la ‘kunata’ kwenye nafasi ya saba linaendelea kuwaandama kwa nguvu.

Ila kwenye kuanza kufunga, wana rekodi yao nzuri tu kwamba kama wakianza kufunga bao, basi ujue hawapotezi labda sare.

Kwani katika mechi 33 walizocheza, wamefanikiwa kushinda 13 na mbili zilizobaki wametoa sare, lakini hakuna timu iliyowafunga au hawajapoteza mchezo wowote baada ya wao kuanza kufungwa.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic