April 9, 2014


Kocha Mkuu wa Azam FC, Joseph Omog, amesema wanahitaji pointi tatu muhimu dhidi ya Ruvu Shooting leo, ili kuweza kujihakikishia nafasi ya ubingwa msimu huu.

Azam FC inashuka dimbani leo kumenyana na Ruvu Shooting katika Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani, mchezo ambao unatarajiwa kuwa na ushindani wa hali ya juu.
Azam inaongoza msimamo wa ligi kwa kuwa na pointi 53, huku ikiwaacha mabingwa watetezi Yanga wakiwa na pointi 49 huku zote zikiwa zimebakiza mechi tatu hadi sasa.

Omog amefunguka kuwa mechi dhidi ya Ruvu itakuwa na umuhimu mkubwa kwao kuweza kushinda ili waweze kupata pointi tatu muhimu zitakazowaweka katika nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa.
“Ligi ni ngumu na ina ushindani mkubwa, kila timu imejiandaa, mchezo wetu wa Jumatano utakuwa muhimu ili kupata pointi tatu za kutupa nafasi ya ubingwa.
“Tunahitaji kushinda ili tuweze kujihakikishia ubingwa, kila mchezaji ana ari na tumejipanga vyema na mazoezi.
“Kila mchezaji yupo fiti, hakuna majeruhi katika kikosi changu cha kwanza,” alisema Omog.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic