April 9, 2014


Uongozi wa Klabu ya Simba umefunguka kuwa, iwapo Azam FC watamhitaji mshambuliaji wao Amissi Tambwe, watakubali kuwapa lakini wabadilishane na Kipre Tchetche.

Azam ilionyesha nia yake ya kumtaka Tambwe kufuatia uwezo anaouonyesha na kudai kuwa ipo tayari kumsajili iwapo watakubaliana na Simba.

Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga, amefunguka kuwa iwapo Azam wapo ‘siriazi’ kumhitaji Tambwe, basi wabadilishane na Tchetche.
“Tutakuwa tayari kumuachia Tambwe kwa sharti la kubadilishana wachezaji kama ilivyokuwa kwa Abdulhalim Humud na marehemu Patrick Mafisango kwa kutupatia Tchetche.
“Sisi tupo tayari iwapo watakuja siriazi kwani tunachoangalia ni maslahi ya timu,” alisema Kamwaga.
Simba iliwahi kubadilishana na Azam kwa kumtoa Humud na kupewa Mafisango ambaye alikuwa msaada mkubwa na kuiwezesha kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2011/2012.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic