April 9, 2014


Uongozi wa timu ya Mbeya City, umesema utahakikisha kuwa katika michezo yao miwili iliyobaki inaziba mianya yote ya hujuma hasa kipindi hiki ambacho vita ya ubingwa imepamba moto.


Mbeya City ambayo imepanda daraja msimu huu, ipo katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 46, saba nyuma ya vinara, Azam FC.

Timu hiyo ambayo imebakiza michezo miwili dhidi ya Mgambo JKT na Azam FC ambayo yote itachezwa katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, imesema ni lazima ihakikishe inashinda mechi hizo.

Katibu Mkuu wa timu hiyo, Emmanuel  Kimbe alisema kwa sasa wanajipanga kupambana na hujuma kipindi hiki ambacho wamebakiza mechi mbili pekee.
Kimbe alisema kuwa, watahakikisha vijana wao wanapambana kwa kujituma na siyo kutumiwa na watu ili kuweza kuihujumu timu, ingawa timu hiyo inazingatia suala la nidhamu na maadili.
“Timu yetu kwa sasa inafanya vitu vyake kwa tahadhari kubwa ili kuweza kuepuka hujuma na maneno ya kashfa kipindi hiki ligi inapomalizika. 
“Ingawa tunawaamini wachezaji wetu lakini ni vizuri tukachukua tahadhari kubwa,” alisema Kimbe.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic