April 9, 2014


Wakati kivumbi cha Ligi Kuu Bara kikitarajia kufikia tamati hivi karibuni huku Azam ikiwa na matumaini makubwa ya kunyakua ubingwa wa michuano hiyo, Kocha Mkuu wa JKT Ruvu, Fred Felix Minziro, ametamba kuisimamisha timu hiyo katika mechi yao ya mwisho ili kuinusuru timu yake na balaa la kushuka daraja.


JKT Ruvu hivi sasa ipo katika hatari kubwa ya kushuka daraja, hivyo inahitaji kufanya vizuri katika mechi zake mbili ilizobakiza kwenye ligi hiyo  dhidi ya Coastal Union na Azam ili iweze kuepukana na balaa hilo linaloinyemelea kwa hivi sasa.
Akizungumza na Championi Jumatano, kocha huyo alisema ni vyema wakiifunga Azam kwenye mchezo wa mwisho ili waweze kuepuka kushuka daraja.

 “Tupo katika hatari kubwa ya kushuka daraja ambayo inatukabili kwa sasa, hivyo tunatakiwa kuwa makini zaidi ili kuepukana na hatari hiyo.

“Hata hivyo njia pekee tuliyonayo ni kushinda mechi zetu zote mbili tulizobakiza kwa sasa dhidi ya Coastal Union na Azam, hivyo inatubidi tujipange na kuhakikisha hatufanyi makosa kama tuliyofanya dhidi ya Yanga,” alisema Minziro.

JKT Ruvu hivi sasa inashika nafasi ya tisa katika msimamo wa ligi kuu ikiwa na pointi 28 juu ya Mgambo JKT (25), Prisons (22), Ashanti United (22), Oljoro(18) na Rhino Rangers (16).


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic