April 15, 2014

MANJI

Mkutano mkuu wa Yanga pamoja utakaoambatana na uchaguzi umepangwa kufanyika Juni 5 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Yanga leo, imeeleza kikao cha Kamati ya Utendaji kilichoketi Aprili 10, makao makuu ya klabu kiliazimia kuwa mkutano mkuu wa Uchaguzi wa Yanga utafanyika tarehe hiyo.

Lakini Yanga ikaeleza kuwa, taarifa kuhusu taratibu za uchaguzi zitatangazwa hapo baadae na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi,  Alex Mgongolwa.
Yanga sasa iko chini ya uongozi wa Yusuf Manji ambaye tayari ametangaza kutogombea tena.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic