April 14, 2014


Kikosi cha wachezaji nyota na wakongwe wa Real Madrid ya Hispania kinatarajia kutua nchini wakati wowote kabla ya mwaka huu kwisha kucheza mechi ya kirafiki.


Kikosi hicho kitakuwa na nyota mbalimbali kama Luis Figo, Michel Salgado, Christian Karembeu na wengine wengi ambao watatangazwa baadaye.
RAYCO GARCIA AKIWA NA SALEH ALLY

RAYCO GARCIA (KULIA) AKIWA NA RONALDINHO WAKATI AKIKIPIGA TIMU YA VIJANA YA BARCELONA
Mchezaji wa zawani wa timu za vijana za Real Madrid na Barcelona, Rayco Garcia amemuambia SALEHJEMBE kuwa mechi hiyo itakuwa ndani ya mwaka huu kama kila kitu kitaenda vizuri.

“Nimefika hapa Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya maandalizi, kuangalia mazingira.
RAYCO GARCIA (KUSHOTO) AKIWA NA LIONEL MESSI

“Lakini kuna watu maalum ambao wanashughulikia mechi hii kufanyika hapa.
“Shirikisho la soka la hapa, pia wana taarifa na wanajua maaendeleo ya suala hili. Hivyo tunataka kuangalia mambo yataenda vipi,” alisema Garcia aliyekuwa ameongozana na beki wa zamani wa Simba, Talib Hilal ambaye pia ni kocha wa timu ya taifa ya ufukweni ya Oman.
Garcia ndiye alisimamia ziara ya timu mbili za Real Madrid na Barcelona za wakongwe ambazo zilicheza mechi ya kirafiki Muscat, Oman mwezi uliopita na Madrid kupoteza kwa mabao 2-1.

Alisema wakongwe wawili, Zinedine Zidane na Roberto Carlos ambao ni makocha wa Real Madrid na Besiktas ya Uturuki, hawatakuwa na nafasi ya kuja na timu hiyo nchini kama mpangilio wa ziara hiyo utawezekana.
RAYCO GARCIA AKIWA  CAMP NOU

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic