June 27, 2014




“UKIANGALIA hivi sasa wanachama wapo mbali sana na klabu yao, kikubwa nitakachoanza nacho ni kuhakikisha ninaiweka klabu pamoja na wanachama wake.


“Nitafanya hayo kwa kushirikiana na wenzangu katika baadhi ya mambo, ikiwemo suala la wanachama kuhakikisha wanashirikishwa katika kuichangia timu yao kwa njia mbalimbali,” hizo ni kauli za mgombea wa nafasi wa ujumbe katika Klabu ya Simba, Collin Frisch.

Collins licha ya kuwa hana jina kubwa kwenye medani ya soka nchini lakini ni mmoja wa waanzilishi wa Kundi la Friends of Simba ambalo limekuwa karibu na klabu hiyo na kushiriki katika shughuli nyingi za klabu.

Frisch anasema, kabla ya kuchukua uamuzi wa kugombea ujumbe Simba, wito mwingi aliupata kutoka kwa matawi mbalimbali ya Simba yaliyokuwa yakimuomba agombee nafasi kubwa zaidi ya hiyo.

“Mimi sasa nimejiajiri na ninafanya shughuli zangu za kilimo,” anasema Frisch na kuendelea: “Naamini huu ndiyo wakati wangu muafaka wa kuwa kiongozi wa Simba kwa kuwa sina majukumu mengi kama ilivyokuwa awali.

“Unajua siku zote uchumi wa klabu unatengenezwa na ufadhili wa makampuni mbalimbali, kampuni zinapenda timu zenye maendeleo na mafanikio.

“Ili uchumi ukue lazima tutengeneze imani kwa wanachama na wadau wetu wote, lakini hiyo itaendana na timu kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa na kitaifa.

“Kwa mfano kipindi ambacho Mohamed Dewji alipoidhamini Simba, timu ilikuwa na mafanikio mbalimbali ikiwemo kufanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa.”

Firsch anaongeza kuwa amepanga kuwa mmoja wa watakaoshawishi uongozi utakaoingia madarakani kuhakikisha wanamiliki mabasi yao kwa ajili ya wanachama wao.

Kocha Profesheno
“Kitaaluma mimi ni kocha na nimesoma kozi nyingi za ukocha kupitia TFF na TAFCA, nina Gredi B ya Preminary.

“Kwa kupitia taaluma yangu ya ukocha, nimepanga kushiriki katika kutengeneza timu nzuri za vijana kuanzia U-17,” anasema Frisch ambaye ni mjumbe wa Lions Club International inayojishughulisha na masuala ya kijamii.
Kamati alizokuwepo Simba
“Niliwahi kuwa kwenye Kamati ya Mashindano ya Simba iliyokuwa na wajumbe kama Hassan Hasanoo, Adam Mgoi, Danny Manembe na Gerald Luqman iliyochaguliwa na Ismail Aden Rage.

“Niliwahi pia kuwa kwenye Kamati ya Usajili chini ya Zakaria Hans Pope, kamati haikufanya vizuri kutokana na kukosa ushirikiano na uongozi wa Rage ambao unamaliza muda wake.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic