June 16, 2014

WAMBURA

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, ameruka kwamba Michael Wambura ambaye ni mgombea wa urais Simba aliyeondolewa kwa mara ya pili, hakuwa meneja wa kampeni zake wakati akiwania kuingia TFF.


Hali imekuwa ngumu na wanachama wa Simba wamemcharukia Malinzi kwamba anaiandama Simba, hasa kutokana na uamuzi wake wa kusitisha uchaguzi uliopangwa kufanyika Juni 29.
 “Jamani mimi sijawahi kutangaza kampeni meneja, nashangaa watu wanasema kuhusiana na huyu bwana (Wambura).
“Kwanza mimi sipendi kutaja majina ya watu, pia ninachopenda ni kuona haki inatendeka,” alisema Malinzi bila ya kusema vipi au wapi haki haijatendeka.
Katika kampeni zake za uchaguzi, hata siku ya mkutano wake wa kwanza na waandishi baada ya kushinda urais wa TFF, Wambura alikuwa kati ya watu waliohudhuria kama rafiki wa karibu wa Malinzi.
Lakini inaonekana kadiri mambo yanavyozidi kuwa magumu, Malinzi anajaribu kutengeneza umbali au kumkana Wambura ambaye inajulikana wazi ni rafiki yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic