June 16, 2014

WANACHAMA WA SIMBA WAKIWA MAKAO MAKUU YA KLABU HIYO HIVI PUNDE WAKIPINGA UAMUZI WA TFF YA MALINZI.



Mambo sasa yamekwisha, wanachama wa Simba wamevunja ukimya na kusisitiza wao watapiga kura za kuchagua viongozi wapya Juni 29 kama ilivyopangwa.


Wanachama hao bila ya woga wametupa lawana nyingi kwa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kupitia Rais wake, Jamal Malinzi kuwa ni wajanjawajanja na wanataka kuihujumu Simba.
WANACHAMA HAO WAKIONYESHA KADI ZAO KUSISITIZA WAO SI WABABAISHAJI ILA NI WANACHAMA, TENA HAI.

Kabla ya kuzungumza na SALEHJEMBE, wanachama hao walifanya vurugu kubwa wakionyesha kuwa na hasira kutokana na taarifa za TFF kuusitisha uchaguzi huo hadi iundwe kama ya maadili.
“Tunapinga, tunajua Malinzi ni Yanga na anataka kuidhoofisha Simba, hatuwezi kukubaliana na suala hilo hata kidogo.
“Tunataka uchaguzi kama kamati ya Ndumbaro ilivyosema. Tutakwenda kupiga kura halafu tuone sasa, huyu Malinzi anatumiwa na Yanga wenzake,” alisema Ally Mohammed Said, mmoja wa wanachama na mashabiki waliojitokeza makao makuu ya Simba leo hii.
Wanachama hao walikuwa wakiimba nyimbo za kumpinga Malinzi na kusema anataka kuona Simba haifanyi usajili ili idhoofike na amekuwa na kampeni ya kutaka kuwaingiza wagombea ambao watafanya kazi pamoja naye na kuidhoofisha Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic