July 23, 2014



Timu ya JKT Ruvu imefanikiwa kumnasa aliyekuwa kipa  wa Yanga wa zamani Benjamin Haule kwa  kumpatia mkataba wa mwaka mmoja wa kuweza kuitumikia klabu hiyo kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.


Kipa huyo aliwahi kuitumikia klabu ya Yanga kipindi cha nyuma, msimu uliomalizika alikuwa akiitumikia timu ya Ruvu Shooting ambayo pia ni ya ligi kuu.

Katibu wa timu hiyo, David Ngaga, alisema kuwa wamewasajili wachezaji kadhaa akiwemo kipa Benjamin Haule ilikuweza kuongeza nguvu katika kikosi chao.

“Ni kweli tumefanikiwa kumsajili kipa Benjamin Haule kwa ajili ya kuitumikia timu yetu msimu ujao, tumempa mkataba wa mwaka mmoja  kwa mwaka mmoja pamoja na wachezaji wengine kama kiungo Mohamed Faki (Ashanti United), Ambrose Morris, Issa Kanduru (Mgambo JKT) Napo Zuberi na Nurdin Mohamed wote JKT Oljoro, hawa kwa miaka mitatu kwa sababu ni askari,”alisema Ngaga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic