July 23, 2014



Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, ameamua kumuangalia zaidi kiungo wake, Uhuru Selemani kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.


Loga ametaka kuona zaidi kiwango chake kabla ya kutoa ruhusa kuwa asajiliwe au la.
Usajili tayari umeongezewa muda kwa siku 14 na Uhuru itabidi achakarike hasa.
"Kama viongozi tumemshauri kocha tumuongezee mkataba mpya Uhuru ili abaki kuendelea kuichezea Simba, hiyo ni kutokana kumkosa kiungo mshambuliaji wa Mbeya City, Kaseke (Deus)," kilieleza chanzo.
“Hivyo kocha ameomba muda kwa ajili ya kumuangalia Uhuru uwezo wake ndani ya uwanja kabla ya kumuongezea mkataba mpya,”kilisema chanzo hicho.
Alipoulizwa Logarusic kuhusiana na taarifa hizo alisema: "Wapo wachezaji wengi ninaendelea kuwangalia katika mazoezi yangu akiwemo Uhuru na yeyote atakayenishawishi nitampa mkataba.
“Bado tuna nafasi za usajili wa wachezaji wa nyumbani kwa ajili ya msimu ujao, nafasi za profesheno zipo mbili ambazo tayari tumetoa mapendekezo ya wachezaji wa kuwasajili kwa ajili ya msimu ujao,”alisema Logarusic.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic