July 7, 2014




Real Madrid imempoteza mchezaji wake gwiji kuliko wote, Alfredo di Stefano ambaye amefariki leo mchana.
Di Stefano mwenye umri wa miaka 88, amefariki dunia akiwa hospitalini jijini Madrid akiwa anapigania uhai wake kutokana na ugonjwa wa moyo.
Ghafla alipata maumivu makali ya moyo akiwa barabarani karibu kabisa na Uwanja wa Santiago Bernabeu unaomilikiwa na Real Madrid.
Ni msiba mkubwa kwa Madrid kutokana na ukubwa wa di Stefano katika klabu hiyo ambayo ilimpa urais wa heshima.
Di Stefano anaaminika ndiyo mchezaji mwenye mafaniko makubwa zaidi akiwa na Real Madrid, ameiongoza timu hiyo kutwaa makombe manane ya La Liga, moja la Copa del Rey na matano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Lakini pia alicheza River Plate ya kwao Argentina na Millonarios ya Colombia na kila nchi amewahi kubeba ubingwa.

MAKOMBE:
REAL MADRID:
-Ligi ya Mabingwa Ulaya (sasa) (Real Madrid, 1956, 1957, 1958, 1959, 1960)
-      Intercontinental Cup (Real Madrid, 1960)

RIVER PLATE
-      
- One America cup (River Plate, 1947)

REAL MADRID

- Ubingwa wa La Liga (Real Madrid, 1954, 1955, 1957, 1958, 1961, 1962, 1963, 1964)
-Copa del Rey (Real Madrid, 1962)


- Ubingwa wa Argentina (River Plate, 1945, 1947)

MILLONARIOS

-Ubingwa wa Ligi Kuu Colombia (Millonarios Bogotá, 1949, 1951, 1952, 1953)


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic