BAADA ya taarifa kuwa Neymar
wa Brazil hatacheza mechi mbili za Kombe la Dunia zilizobaki, hisia tofauti za
mashabiki zilitawala na sherehe za Brazil kufuzu hatua ya nusu fainali,
hazikuwa gumzo kubwa.
Beki wa Colombia, Juan Camilo
Zuniga ,28, akachukua nafasi, mashabiki wa soka katika vijiwe mbalimbali na
mitandano ya jamii wamekuwa wakitofautiana kuhusiana na faulo aliyoifanya
Zuniga dhidi ya Neymar na kumvunja mfupa mdogo wa uti wa mgongo.
Mashabiki wengi wa Tanzania,
wanaamini Zuniga ambaye anakipiga Napoli ya Italia si mtu mzuri kwa kuwa
amewanyima burudani ya kumuona Neymar ,22, katika mechi mbili zilizobaki, yaani
nusu fainali na fainali au mshindi wa tatu.
Lakini kwa wale wa Brazil,
hisia ni zaidi ya kawaida, Zuniga ni adui wa taifa, Waingereza wanasema Public
enemy. Hawataki kumuona na wako ambao wametishia hata kumtoa roho.
Haraka msafara wa Colombia
uliongezewa ulinzi baada ya kusambaa haraka kwa taarifa hizo na zile za Neymar
kusafirishwa kwa helkopta hadi Sao Paulo ambako anatibiwa na baadaye atakwenda
kupumzika nyumbani.
Wabrazil kadhaa walisafiri
hadi kwenye hoteli waliyofikia Colombia, ingawa hawakuweza kukaribia lakini
waliimba na kumkashifu.
Tayari Zuniga anayekipa
Napoli ya Italia ameomba radhi, lakini ndiyo amesababisha gumzo kubwa na wengi
wanaamini alifanya makusudi wakitumia kigezo cha faulo nyingine aliyoifanya
siku hiyo.
Zuniga alimrukia
mshambuliaji wa Brazil, Hulk wakati akiambaa na mpira. Mguu wake ulikwenda moja
kwa moja kwenye goti. Mashabiki hao wanasema Zuniga alipania kumuumiza mchezaji
yoyote wa Brazil.
Baadhi wameweka picha za mtu
akichomwa moto na kuwataka mashabiki wa Brazil popote walipo kummaliza beki
hiyo, lakini wengine wameweka picha za vijana wakiwa na bunduki na kusema
Colombia wamezoea vurugu na vita na wanashauri Shirikisho la Soka la Kimataifa
(Fifa) kuwaondoa ili waingie kwenye mashirikisho ya wapiganaji kwa kutumia
silaha, kama yatakuwepo.
Ukiangalia kwa makini katika
faulo alizocheza kupitia video, zinaonyesha kuna walakini na huenda Zuniga
alipania kufanya jambo ambalo si zuri, kweli.
Faulo ya Hulk:
Hulk alikuwa amekimbia na
kuudokoa mpira hata kabla ya Zuniga kuruka, lakini anaonekana akiwa ameamini
mpira ule hawezi kuuwahi na kilichobaki ni kucheza na mwili wa mshambuliaji
huyo.
Kweli Zuniga anaruka mguu
wake ukiwa umelenga goti la Hulk, anafanikiwa kumpata lakini bahati nzuri
hajaumia kama ilivyo kwa Neymar.
Faulo Neymar:
Inawezekana Zuniga hakujua
kiasi gani atamuumiza nyota huyo wa Brazil, lakini hakuna ubishi alijua
anakwenda kufanya madhambi na si kuchukua mpira.
Zuniga alikuwa nyuma ya
Neymar ambaye aliuficha mpira mbele yake, kwa kuwa alikuwa amegeukia kwenye
lango lao, Zuniga alitakiwa kutumia akili kumpokonya mpira au kumpa presha
auotoe.
Yeye akamrukia moja kwa moja
na hata wakati Marcelo na James Rodriguez wakijaribu kumsaidia, Zuniga
aliendelea na mambo yake kama vile hana habari.
Hoja ni hivi, wakati
Colombia ilikuwa nyuma kwa bao moja, si lahisi mchezaji kufanya faulo ya
kipuuzi kama ile ya Zuniga, badala yake kwa dakika tatu zilizobaki, alikiwa
kupambana kuupata mpira bila kufanya madhambi ili washambuliaji na kusawazisha!
Picha:
Picha ya tukio ambalo Zuniga
anamrukia Neymar mgongoni na kumvunja mfupa mdogo wa uti wa mgongo, ndiyo
imeangaliwa zaidi kwa saa 24 baada ya tukio.
Awali picha iliyokuwa
kiburudisho zaidi ni ile ya Robin van Persie wa Uholanzi akifunga bao kama vile
anapaa, ilikuwa mechi dhidi ya Hispania.
Picha ya Zuniga na Neymar
imeangaliwa na mashabiki wanaokosiwa kufikia milioni 55, wakati ile ya van Persie
iliangaliwa na mashabiki milioni 48, ndani ya saa 24.
0 COMMENTS:
Post a Comment