MUSOTI AKIWA NA VIONGOZI WA ZAMANI WA SIMBA, MTAWALA NA MZEE KINESI |
Beki kisiki wa Simbam, Donald Musoti, ameungana na kocha Zdravko Logarusic kuwa aongezwe beki mwingine mzoefu wa kati.
Loga alipendekeza hilo katika ripoti yake na kusisitiza Simba inahitaji beki mzoefu mmoja.
Musoti alisajiliwa na Simba msimu uliopita
ambapo amekuwa na msaada mkubwa kwa timu hiyo tangu alipojiunga nayo.
Beki huyo Mkenya alisema klabu kubwa kama ya Simba haistahili kuwa na mchezaji
mmoja tegemezi katika nafasi moja na badala yake uongozi ungesajili wachezaji
zaidi ya mmoja katika nafasi moja ili kuleta ushindani.
“Unajua klabu kubwa kama ya Simba haipaswi
kuwa na mchezaji mmoja wa kutegemewa katika namba moja na badala yake kuwe na
wachezaji wawili ama watatu ili kusaidiana, wakifanya hivyo timu ndiyo ninapokuwa
na ushindani.
“Mfano mzuri msimu uliopita timu ilishindwa
kuwa katika kiwango kizuri sababu kubwa ikiwa ni hiyo, ilikuwa akikosekana mtu
basi timu inayumba na kushindwa kucheza kama inavyotakiwa.
“Iliniuma kumaliza katika nafasi ya nne kwa
timu kubwa kama Simba ni vyema
tukajipanga upya kwa msimu ujao,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment