Wachezaji
wa Simba, kwa nyakati tofauti wamesema mazoezi ambayo hufanya ufukweni au gym
chini ya Kocha Msaidizi, Selemani Matola si mchezo.
Mmoja
ameiambia SALEHJEMBE, yale mazoezi si mchezo huku akisema Matola ‘atawaua’.
Lakini
kila mmoja wao akasisitiza kuwa anachofanya Matola ni faida ya kwao baadaye.
“Kweli
ni mazoezi magumu sana, mfano ufukweni, wakati mwingine unajisikia kama unataka
kufa, hahaha,” alisema mmoja.
Lakini
mwingine ambaye ni kiungo kinda, aliungana na mwenzake na kusema mazoezi hayo
ya ufukweni na gym ni makali sana.
Akasisitiza
wanalijua hilo ndiyo maana wamekuwa wakifanya kwa juhudi wakijua ligi itakuwa
na ushindani sana.
Matola
ndiye amekuwa akiongoza mazoezi ya ufukweni na gym wakati Kocha Mkuu, Zdravko
Logarusic amekuwa akiungana naye kwenye mazoezi ya jioni.
0 COMMENTS:
Post a Comment