Ili kuondoa utata kwamba huenda nani ataanza katika mechi ya kesho ya
Super Cup kati ya kipa Iker Casillas na yule mpya Kyler Navas, Kocha wa Real
Madrid, Carlo Ancelotti ameweka wazi kabisa kwamba Casillas ndiye atacheza.
Mechi hiyo ya Spanish Super Cup dhidi ya wapinzani wao wakubwa,
Atletico Madrid na tayari imekuwa gumzo.
“Tumejiandaa kwa dakika 180 za mechi hiyo, tutaanza na 90 halafu
tutamalizia na kipande cha pili. Tunataka kufanya vizuri katika mechi zote,”
alisema Ancelotti.
Makipa: "Iker ndiye atakayecheza na mengine tyatafuatia.”
Di María: "Siwezi kuzungumzia kuhusiana na Di Maria, ninahofia kuchelewa
nilicholenga kuhusiana na mechi ya kesho.”
James: "Hajakosa chochote kama ilivyoelezewa, alijitahidi na tunaona
msaada wake unahitajika, tunamhitaji.”
Diego López: "Hakuna aliyeamua kumuondoa Diego López, binafsi ndiye aliamua kubadili mazingira, tulikuwa na makipa wawili msimu uliopita, sawa na msimu huu. Hakuna tatizo.
Diego López: "Hakuna aliyeamua kumuondoa Diego López, binafsi ndiye aliamua kubadili mazingira, tulikuwa na makipa wawili msimu uliopita, sawa na msimu huu. Hakuna tatizo.
Kroos: "Anaongeza kiwango cha timu, amekuwa changamoto na uzoefu wake
umekuwa msaada katika kikosi chetu.”
Mfumo: "Tuna staili yetu, ile ya msimu uliopita pia msimu huu. Kwa
kifupi hii ni Madrid, ileile."
0 COMMENTS:
Post a Comment