Kocha Diego Simeone ameizungumzia mechi ya kesho na kusema wapinzani
wake, Real Madrid wameimarika zaidi.
Simeone amesema Madrid wameimarika zaidi kupitia kiungo wao mpya Toni Kroos,
raia wa Ujerumani ambaye atafanya mechi hiyo izidi kuwa ngumu.
Kroos amejiunga na Madrid akitokea Bayern Munich na alicheza katika mechi ya Super Cup ya Ulaya dhidi ya Sevilla ambayo walishinda kwa mabao 2-0, yote yakipachikwa na Ronaldo.
Timu hizo zinakutana katika mechi ya Super Cup ya Hispania ambaye
huwakutanisha bingwa wa La Liga na Copa del Rey ikiwa ni maalum ya kufungua
msimu.
Pia alisema, mshambuliaji Gareth Bale amezidi kuwa bora kuliko msimu
uliopita, hali ambayo itaongeza ushindani zaidi.
Washambuliaji: "Tunaendelea kucheza kwa aina ya mtindo wetu hata kama tutakuwa
hatuko na wachezaji wote, ni mmoja tu, Diego Costa ndiye tutamkosa. Ila Jiménez
yuko fiti na anatufanya tuamini kama hakuna tatizo.”
Goalkeepers: "Moyá atacheza, pia Oblak ambaye yuko fiti, hivyo hatuna hofu. Kwa
kifupi tuko tayari kwa ajili ya mechi hiyo."
0 COMMENTS:
Post a Comment